WAKALA WA VIPIMO YATOA ELIMU KWA BAADHI YA WATUMISHI WA SHIRIKA LA UZALISHAJI MALI JESHI LA KUJENGA TAIFA (SUMA JKT).

Imewekwa:May 14, 2024

Katika kuendeleza juhudi zake za kuwafikia wadau na kuwapa elimu ya matumizi sahihi ya vipimo, Wakala wa Vipimo (WMA) imewapa elimu hiyo baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya SUMA JKT waliopo ilala NSSF Mafao leo tarehe 14 Mei, 2024.

Akitoa elimu katika sehemu ya ofisi za mfuko wa taifa wa hifadhi ya jamii (NSSF) Ilala Jijini Dar es salaam,Afisa Vipimo Bwana Yahaya Tunda amewaelimisha wafanyakazi hao namna ya kutambua vipimo sahihi vilivyohakikiwa na Wakala wa Vipimo (WMA) na matumizi sahihi ya vipimo hivyo katika maeneo mbalimbali ya biashara ili kuleta haki na usawa kati ya mnunuzi na mtoa huduma.

Bwana Yahaya ameongeza kuwa, Wakala wa Vipimo inaendelea kujikita katika kutoa huduma bora sanjari na elimu ya vipimo kwa wadau na wananchi kwa ujumla ili kukuza ufanisi katika sekta ya vipimo.

Kwa upande wake msimamizi wa Shirika la Uzalishaji Mali Jeshi la Kujenga Taifa (SUMA JKT) jengo la NSSF Ilala, Bwana Ernest Baraiga ameishukuru Wakala wa Vipimo kwa kuwapa elimu na kuwajengea ufahamu juu ya matumizi sahihi ya vipimo katika maeneo mbalimbali na kuahidi kutoa ushirikiano kwa Wakala katika Nyanja mbalimbali.

Wakala wa Vipimo kupitia sehemu yake ya mawasiliano na mahusiano kwa umma imekuwa ikitoa elimu na kukutana na wananchi na wadau katika majukwaa mbalimbali ya uelimishaji ili kujenga ufahamu na kutanua wigo wa matumizi sahihi ya vipimo katika maeneo ya biashara,afya,mazingira na usalama na kuleta maendeleo kwa t