WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA ATEMBELEA KITUO CHA UHAKIKI WA VIPIMO MISUGUSUGU
Imewekwa:July 11, 2024
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Selemani Jafo (Mb) ametembelea kituo cha uhakiki wa vipimo misugusugu mkoani Pwani na kupokelewa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo (WMA) ndugu. Alban Mark Kihulla.
Akiongoza
ujumbe kutoka Wizara ya Viwanda na Biashara, waziri Dkt. Jafo ametembelea jengo
linalofanya uhakiki wa dira za maji, jengo la kuhakiki mita za umeme, pamoja na
sehemu ya kufanyia uhakiki wa matenki ya magari yanayotumika kusafirishia vimiminika
ndani na nje nchi.
Katika
ziara hiyo, waziri Dkt. Jafo ameshuhudia utendaji kazi wa mitambo mbalimbali ya
uhakiki wa dira za maji na mita za umeme unaofanywa na Wakala wa Vipimo katika
kituo hicho cha uhakiki wa vipimo misugusugu.
Aidha,
Waziri Dkt. Jafo amepokea maelezo kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa
Vipimo ndugu Alban Kihulla juu ya utendaji kazi wa WMA katika maeneo mbalimbali
na takwimu jumuishi za miaka mitatu (2022 -2024) ya utendaji kazi wa WMA.
“Mheshimiwa
Waziri, Dkt. Selemani Jafo karibu sana katika kituo chetu cha uhakiki wa vipimo
kilichopo hapa misugusugu mkoani Pwani, kituo hiki ni maalum kwa uhakiki wa
dira za maji, mita za umeme na Magari yanayotumika kusafirisha vimiminika.
Katika kituo hiki tuna mitambo mikubwa miwili ya uhakiki wa mita za umeme na
kila mtambo unahakiki mita 20 kwa mara moja ambapo kwa siku tunahakiki mita
1200 za umeme, lakini pia tuna mtambo mwingine wa kuhakiki mita za umeme uliopo
mkoani Kilimanjaro. Mhe.Waziri hadi sasa tumekwisha hakiki mita 4500 kutokana
na mitambo hii ya kisasa tuliyonayo” alisema ndugu Kihulla akimueleza Waziri,
Dkt. Jafo.
Ndugu
Kihulla ameongeza kuwa, WMA inafanya uhakiki wa mita za umeme na dira za maji
kwa ufanisi mkubwa lengo likiwa ni kusimamia haki na kuleta usawa katika
biashara baina ya mtoa huduma na mteja na kuepusha madhara yatokanayo na
matumizi yasiyo sahihi ya vipimo.
Ndugu
Kihulla amemueleza Mhe.Waziri Dkt. Jafo kuwa Wakala wa Vipimo inaendelea
kujikita katika utoaji wa huduma bora na zenye ufanisi kwa kuwafikia wananchi
kwa upana wake kutokana na kuwepo kwa ofisi za Wakala wa Vipimo katika mikoa
yote ya Tanzania bara, lakini pia uwepo wa ofisi za WMA katika mipaka yote ya
nchi kama namanga,holili,sirari,tarakea na tunduma ambapo bidhaa zinazoingia
kupitia mipakani uhakikiwa kabla haijaingia nchini.
Aidha,
ndugu Kihulla ameongeza kuwa, WMA inaendelea kutekeleza majukumu yake muhimu na
ya kimkakati kwa kujiwekea malengo na kuyafikia malengo hayo kwa wakati
unaotakiwa.
Ndugu
Kihulla amesema kuwa “ katika miaka mitatu iliyopita, mwaka wa fedha 2021-2022
Wakala wa Vipimo ilifikia lengo na hata kuvuka kwa asilimia moja katika
ukusanyaji wa ada na mapato yanayotokana na utekelezaji wa majukumu ya msingi
ya WMA, mwaka wa fedha 2022-2023 WMA imefikia
malengo yake kwa asilimia 98 na mwaka wa fedha 2023-202 wakala imefikia malengo
kwa asilimia 83.5. Katika mwaka wa fedha uliopita (2023-2024), WMA ilifanikiwa
kukusanya mapato kiasi cha shilingi Bilioni 31.616 ya mapato yatokanayo na ada
mbalimbali zinazokusanywa na wakala, mapato hayo ni asilimia 99.6 ya ufikiwaji
wa malengo ya WMA katika mwaka huo wa fedha.Lakini pia WMA imepanga kukusanya
Bilioni 39.65 katika mwaka huu mpya wa fedha”
“Tutaendelea
kuangalia fursa mbambali za ukuaji katika muktadha wa vipimo, tutaendelea kuchangia
katika mfuko wa Serikali kwa wakati, na kwa bahati nzuri Mheshimiwa Waziri sisi
WMA tumeshinda tuzo hivi karibuni ya taasisi inayotoa gawio kwa serikali kwa
wakati, tuzo hii tulikabidhiwa na Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Tumejipanga kufanya kazi kwa bidii na kufikia malengo yetu.” Alisema ndugu
Kihulla.
Sanjari
na hayo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo,ndugu Alban Kihulla amemueleza
Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Seleman Jafo changamoto mbalimbali za
WMA ikiwemo upungufu wa watumishi katika taasisi hiyo ambapo ina watumishi 270
kati ya 581 wanaotakiwa na taasisi hiyo na hivyo kuwepo na upungufu wa
watumishi 311.
Aidha,
Ndugu Kihulla ametanabaisha malengo ya WMA kwa mwaka huu wa fedha kuwa ni kununua
vifaa na mitambo mipya na ya kisasa ili kuendana na kasi ya maendeleo ya
teknolojia na ukuaji wa biashara kwa ujumla, kuwajengea uwezo na uzoefu mkubwa
watumishi wa WMA katika nyanja mbalimbali ili kutoa huduma bora na kwa ufanisi
mkubwa kwa wananchi, lakini pia kujiimarisha katika mifumo yake na kuongeza
ufanisi katika kusomana kwa mifumo na wakuu wa taasisi zingine za serikali
katika utoaji wa huduma.
Kwa
upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Vipimo Profesa Eliza
Mwakasangula amemshukuru Waziri, Mhe. Dkt. Jafo na ujumbe wake kwa kuitembelea
Wakala wa Vipimo na kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na taasisi hiyo
katika kuwahudumia wananchi.
Profesa
Eliza Mwakasangula amemuomba Waziri Mhe, Dkt. Jafo kusimamia mchakato wa kuifanya
WMA kuwa Mamlaka ili kutanua wigo na ufanisi katika utendaji kazi wake na kuwahudumia
wananchi sanjari na kuchochea maendeleo ya taifa kwa ujumla.
Kwa
upande wake Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt, Seleman Jafo amemshukuru
Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo ndugu Alban Kihulla na watumishi wa
wakala kwa kumpokea vyema na kumpitisha katika maeneo mbalimbali ya kiutendaji.
“Leo
nimekuja kuwatembelea ndugu zangu wa Wakala wa Vipimo katika kituo chenu cha
uhakiki wa vipimo cha misugusugu kwa lengo kufahamiana na ninyi kwanza, lakini
pia mmenipitisha kwenye maeneo ya utendaji kazi, mnafanya kazi nzuri na
ninawapongeza sana”
“mimi
ni mtu wa kazi kwa hiyo Afisa Mtendaji Mkuu naomba sasa mjipange vyema kwa
sababu kazi ndo imeanza na tukutane eneo la kazi (site)” amesema Mhe. Jafo.
Katika
hatua nyingine Mhe. Dkt Jafo amemuagiza Afisa Mtendaji Mkuu wa WMA kuhakikisha
mita zote za umeme na dira za maji zinahakikiwa na WMA na kupelekwa kwa
wananchi katika muda muafaka bila ya kuwepo na kikwazo chochote.
“Nakuagiza
ndugu Afisa Mtendaji Mkuu, hakikisha mita zote za umeme na maji zinahakikiwa
hapa bila ya kikwazo chochote, ofisi yangu iko wazi muda wote leteni kanuni
zozote zitakazofanya zoezi la uhakiki kufanikiwa kwa asilimia zote. Lakini pia
hakikisha unakaa na taasisi zingine kama TANESCO na zingine mjue namna bora ya
kufanya kazi katika hilo, baada ya muda nitahitaji ripoti ya hatua mliyofikia”
alisema Mhe. Jafo.
Aidha
Mhe. Jafo amemuelekeza Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vipimo kuelekeza nguvu
zake katika mapambano dhidi ya ufungashaji holela wa mazao ( lumbesa),
ufungasshwaji wa saruji, nondo na mabati ili kupambana na wafanyabiashara na
wazalishaji wote wenye nia ovu ya kuchezea vipimo kwa manufaa yao binafsi.
Waziri Mhe. Dkt. Jafo ameitembelea WMA ikiwa ni taasisi ya pili kuitembelea kati ya taasisi 13 zinazounda Wizara ya Viwanda ya Biashara tangu kuteuliwa kwake kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara huku akisisitiza utendaji kazi bora na wenye tija kwa maendeleo y