Kurugenzi
Wakala wa Vipimo ina kurugenzi mbili;
KURUGENZI HUDUMA ZA BIASHARA
Kusimamia kwa usahihi rasilimali za taasisi na kuhusisha matumizi ya Tehama kwa lengo la kutoa huduma bora na kuleta ustawi wa taasisi. Hivyo, Kurugenzi hii;
1. Utoa
ushauri juu ya ufanisi wa Taasisi na namna bora ya kuboresha utoaji wa huduma;
2. Uwezesha
Wakala kutekeleza Sera na majukumu ya Kisheria;
3. Uandaa
na kutoa ushauri wa Kitaalam juu ya mifumo ya
usimamizi wa fedha na rasilimali za Wakala;
4. Kusimamia masuala mtambuka yanafanyiwa kazi
katika Mpango Mkakati wa Wakala;
5. Kusimamia matumizi mazuri ya fedha na mali za Wakala pamoja na
6. Kuratibu uandaaji wa Mpango Mkakati na Bajeti katika Wakala.
KURUGENZI HUDUMA ZA UFUNDI
1. Kusimamia utendaji kwenye shughuli za utekelezaji wa Sheria ya vipimo2. Kutengeneza na kufanya mapitio ya miongozo inayosimamia matumizi ya vifaa na utoaji wa huduma za kiufundi
3.Kutoa taarifa za utendaji kwenye masuala ya ufundi
4. Kubuni na kuweka mazingira rafiki ya utoaji wa huduma ili kwenda sambamba na teknolojia mpya za vipimo
5. Kushiriki kwenye majukwaa ya kikanda na kimataifa yanayohusu vipimo na kusamba taarifa zake
6. Kubuni na kuweka mipango ya mwelekeo wa Wakala katika masuala ya ufundi
7. Kutekeleza majukumu mengine atakayopangiwa na Afisa Mtendaji Mkuu
| ReplyForwardAdd reaction |