Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Wakala wa Vipimo
Vipimo Sahihi na Vya Kuaminika kwa Wote
Background

Kurugenzi

Chunguza kurugenzi mbalimbali zinazoendesha misheni na shughuli za Wakala wa Vipimo.

Kurugenzi ya Huduma za Ufundi

Kurugenzi
01

Kusimamia utendaji kwenye shughuli za utekelezaji wa Sheria ya vipimo

02

Kutengeneza na kufanya mapitio ya miongozo inayosimamia matumizi ya vifaa na utoaji wa huduma za kiufundi

03

Kutoa taarifa za utendaji kwenye masuala ya ufundi

04

Kubuni na kuweka mazingira rafiki ya utoaji wa huduma ili kwenda sambamba na teknolojia mpya za vipimo

05

Kushiriki kwenye majukwaa ya kikanda na kimataifa yanayohusu vipimo na kusambaza taarifa zake

06

Kubuni na kuweka mipango ya mwelekeo wa Wakala katika masuala ya ufundi

07

Kutekeleza majukumu mengine yatakayopangwa na Afisa Mtendaji Mkuu

Kurugenzi ya Huduma za Biashara

Kurugenzi
01

Kusimamia kwa usahihi rasilimali za taasisi na kuhusisha matumizi ya Tehama kwa lengo la kutoa huduma bora na kuleta ustawi wa taasisi.

02

Kutoa ushauri juu ya ufanisi wa Taasisi na namna bora ya kuboresha utoaji wa huduma.

03

Kuwezesha Wakala kutekeleza Sera na majukumu ya Kisheria.

04

Kuandaa na kutoa ushauri wa Kitaalam juu ya mifumo ya usimamizi wa fedha na rasilimali za Wakala

05

Kuratibu uandaaji wa Mpango Mkakati na Bajeti katika Wakala