Uhakiki wa Mita za Mtiririko
Maelezo ya kina kuhusu mchakato wetu wa uhakiki.
Mita za mtiririko hutumika kupima kasi ya mtiririko wa vimiminika au gesi kwenye mabomba, mara nyingi katika viwanda, maghala ya mafuta, na mifumo ya usambazaji maji. Wakala wa Vipimo huhakikisha mita hizi zinapima kwa usahihi ili kuepuka hasara na kuhakikisha biashara ya haki.
Hatua za Mchakato wa Uhakiki
Hatua 1
• Mita za kumbukumbu za viwango hutumika kupima usahihi wa mita ya mtiririko.
Hatua 2
• Ikiwa kuna hitilafu, mita inarekebishwa au kubadilishwa.
Hatua 3
• Mita zilizoidhinishwa hupigwa muhuri wa uthibitisho ili kuzuia udanganyifu.
Hatua 4
• Ukaguzi wa mara kwa mara hufanyika ili kuhakikisha usahihi unaendelea.